Proverbs 7:10-15


10 aNdipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,
hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

11 b(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,
miguu yake haitulii nyumbani;

12 cmara kwenye barabara za mji,
mara kwenye viwanja vikubwa,
kwenye kila pembe huvizia.)

13 dHuyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,
na kwa uso usio na haya akamwambia:


14 e“Nina sadaka za amani nyumbani;
leo nimetimiza nadhiri zangu.

15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;
nimekutafuta na nimekupata!
Copyright information for SwhKC